Unajua kutengeneza pesa kwenye uchumi mpya?





Ni mambo ya watoto!
Siku Fulani iliyopita, rafiki yetu mpendwa alitutembelea nyumbani kwetu Afrika ya Kusini. Kijana wake wa miaka 14 alizaliwa karibu sawa na mtoto wetu mdogo wa kike, na walisoma chekechea pamoja. Nitamwita “John” kwa ajili ya kisa hiki kidogo, ambacho kwa namna nyingine ni kweli.
Mama yake alianza kwa majivuno na kusema, “John ni mfanyabiashara hakika,” kiuhalisia mama wote wanjivunia watoto wao, kwa nini yeye awe tofauti?
Basi, akaendelea kusema, “Wakati mwingine anatengeneza hadi randi 5000 kwa kutengeneza kurasa za mitandao ya kijamii na kuziuza.
“Anafanya nini?” Nilishangaa.

“Ah, hiyo sio kitu. Anafanya hivyo akihitaji fedha za ziada.”
“Sawa… nini kingine anachofanya?”
“Hivi karibuni alifanya mazungumzo kwa ajili ya kitu Fulani cha kuchezea kutoka India, ili kukisambaza Afrika Kusini”
“Alifanya nini?!”
Akasema, “Huwa anakwenda kwenye Internet na kufanya utafiti wa bidhaa na bei, na kutafuta vyanzo vya bei nafuu kwa ajili ya vitu kama ubao wa kuchezea Kriketi, na vitu vingine ambavyo watoto wanapenda.”
Nikauliza kwa upole ili tu nijihakikishie, “Unazungumzia John na sio baba yake?”
“Wakati mwingine John humuomba baba yake amuwakilishe, pale anapohitaji mtu mzima.”
“Enhee!. . . Kwa hiyo anamuajiri baba yake mwenyewe!”
“Angalia, John sio mtoto pekee anayefahamu jinsi ya kutengeneza pesa kutoka kwenye mtandao.”
Kufikia hapo, nikacheka na kusema: “kufikia hapo upo sahihi! Joe Gebbia, Brian Chesky, Nathan Blechaczyk (mmoja wa walio anzisha Airbnb): Evan Spiegel, Reggie Brown na Bobby Murphy (Walioanzisha Snapchat) na pia, Mark Zuckerberg!”
“Hawa jamaa walikuwa watoto tu kulinganisha na watu kama mimi. Na bado walikuwa wamekwisha kujenga biashara ambazo ni kubwa kuliko pato la taifa la nchi nyingi za Kiafrika!”
Lakini hapa kuna jambo la “kushangaza”
“John” ni mtoto wa kiafrika. Kama vile Anesi, na kaka yake, Osine, kutokea Nigeria ambao niliwazungumzia mwaka 2015. Watoto ambao walitengeneza kitafutaji (Browser) Hata kabla hawajaingia umri wa balehe?
Hii inamaanisha kwamba Zuckerberg anayefuata labda anaishi nyumbani kwako, akizunguka tayari akiwa anacheza na Lego na labda akifikiria kuhusu maroboti au zaidi!
Nyumbani kwangu mwenyewe, binti yetu mdogo huwa anafanya mambo yote “ya kiteknolojia” wakati watu walipomaliza Tovuti ya Kwese, nilimwita na nikamuuliza, “hii ina iko vizuri?”
Alienda kwenye kona akasema, “iko poa sana, lakini ningeweza kubadilisha hiki na hiki.”
Nikamwambia, “ngoja nitafute pa kuandika mwanangu.”
Akasema, “utanilipa!”
Nikamwambia, “sema gharama yako.”
Nikauliza swali rahisi: “unafahamu kweli jinsi ya kutengeneza fedha kwenye uchumi huu mpya?”
Katika uchumi mpya, itakuwa ni kuhusu uwezo wetu wa kuachilia mitizamo ya zamani kuhusu mali, na jinsi ya kutengeneza mali. Lazima si tuwawezeshe tu watoto wetu; lazima tuwaamini katika siku zetu zote zijazo.
Mwisho wa juma hili, fanya mahojiano kidogo na uchunguze kile ulichofanya na simu yako ya smartphone:
Ni tovuti gani ulizotembelea, na kwa nini?
v Je! Ilikuwa kwa ajili ya kutafuta kitu?
v Je! Ilikuwa kwa ajili ya kuuza au kununua kitu?
v Ili kuwa kwa ajili ya kuburudika?
v Je! Ilikuwa ni kwa ajili ya kuwasiliana na marafiki na familia?
Kama kimsingi ilikuwa ni kwaajili ya kuwasiliana na watu, au ubadilishe tabia yako, au itakubidi umfanyie kazi “John” siku moja … (Lakini haitakuwa mbaya, maana angalau utakuwa na kazi.)
Katika mambo yote unayofanya kwenye mtandao, je ulitengeneza fedha yoyote, endeleza kazi yako au piga teke ili kuanzisha ule mwanzo wa biashara yako?
Ninamfikiria John mdogo. Ana miaka 14, na tayari ameshaelewa uchumi mpya. Wow!

Hebu na tuingie kazini! Tuna bara zima la kufanyia marekebisho … Tena haraka!

Comments

Popular Posts