Vifaa Vyako vya Kazi

Jitayarishe
kufanya mabadiliko katika kazi yako.
Siku zote wekeza
katika “vifaa vyako vya kazi”
Muda mfupi baada ya mimi kumaliza shahada yangu ya uhandisi
huko Uingereza, ilinibidi kufanya kazi katika kituo cha uzalishaji huko
Uingereza ili kupata “uzoefu wa kivitendo” kama walivyoiita kazi hiyo. Mafundi wengi
ambao walikuwa pale kwa miaka mingi, walikuwa na ratiba Fulani ambapo niliweza kupata
baadhi ya “vitendo na uzoefu wa maisha halisi.”
Inashangaza mara zote kwamba ni kanuni za muhimu kiasi gani
unaweza ukapata, ambazo hata ukienda kufanya kitu kingine tofauti kabisa katika
maisha yako zitakufaa.
v Jisikie
kiburi juu ya vifaa vyako vya kazi.
Kila fundi alikuwa na “boksi la vifaa vya kazi” ambavyo
walivitunzaa kwa upendo. Ilikuwa ni kama “ibada ya mwisho.” Ilipofika mwisho wa
kila siku, walikuwa wakiringishiana vifaa vyalivyoweza kupata, na kile
walichofanyia vifaa hivyo. Walisafisha vifaa vyao mara baada ya siku kuisha.
Kununua na kuwekeza katika vifaa vilivyo bora ili ichukuliwa
kuwa wajibu binafsi wa fundi yoyote, na sio mwajiri.
“Ninalisha watoto wangu kwa vifaa hivi, au sio?” mmoja wao
aliwahi kunieleza hili kwa kiingereza chake kibovu.
Turuke mbele:
Mara zote nilikuwa nikipoteza kalamu yangu ya plastiki. Kisha
mtu mmoja akaniambia, “usingeipoteza kama ungewekeza kwenye kalamu sahihi.”
“Dah!” nikawaza. “hii ni kama vile mafundi wazungu wa zamani
na vifaa vyao.”
Siku ile, niliondoka nikaenda kujinunulia seti nzuri ya
kalamu. Na mara moja nikaacha kupoteza kalamu!
Swali: “Vifaa vyako vya kazi” ni vipi?
Je! Una komputa? Kila mtu anayeendesha biashara ya kisasa,
au anafanya kazi katika utaalamu fulani, lazima awe na laptop.
Komputa sio hata “kifaa” ni “boksi la vifaa” ambalo ndani
yake mnawekwa vifaa vyote vya kisasa.
Je! Upo kwenye mtandao? Je! Una mtandao kweenye biashara
yako na nyumbani kwako?
*kama sio, ni bora uuze gari lako, kama unalo, na utembee,
lakini lazima uwe na komputa na uwe kwenye mtandao wakati wote.
*kama una nyumba kubwa, ina hekima zaidi katika ulimwengu wa
sasa kuwa na nyumba ndogo yenye mtandao, kuliko nyumba kubwa isiyo na mtandao.
*Ingeonekana kuwa na hekima zaidi kuwa na gari dogo, au
kutokuwa nalo kabisa,na uwe na uwezo wa kumudu komputa na Mtandao kwa ajiliya
biashara na familia yako, kuliko kuwa na gari kubwa au vyovyote vile.
*wale wanaoelewa kile ninachozungumza hapa wapo kwenye
nafasi nzuri ya kufanya mabadiliko katika kazi zao kulingana na inavyohitajika
kama matokeo ya mabadiliko ya ghafla kazini, na kwenye kazi tunayofanya.
Kazi yoyote unayofanya, au unayopanga kufanya siku za
mbeleni, unapaswa kukuza “boksi lako la vifaa” kulingana na mabadiliko ya
nyakati zijazo. Ninataka uwe umejiandaa. Kumbuka nilichowahi kusema kuhusu
mtazamo wako? Na kuhusu kufikiria mwisho wa upeo wa mwisho wa upeo wa leo?
Kama nilivyokwisha wahi kusema, “mapinduzi ya mitandao ya
simu” yamekwisha kusafisha njia kwa ajili ya “Mapinduzi ya kimtandao.” Kama mtandao
ungekuwa ni bahari, basi kile unachokiona leo ni ufukwe tu. Mtandao
utabadilisha hata vijiji vyetu. Siku zijazo, mashine ya kusaga mtaani kwako
itatumia mtandao, hata kuweka oda na kutunza kumbukumbu ya rasilimali. Hata shule
ya kijiji itabadilishwa kwa mtandao.Utaona yakitokea. Sehemu Fulani, mtu Fulani tayari anahangaika kutafuta suluhisho. Ni miaka kumi tu iliyopita, kama ningepaswa kukwambia, “Wanavijiji katika sehemu za ndani kabisa mwa Afrika na Tanzania wangekuwa tayari kupokea pesa kutoka sehemu yoyote ulimwenguni ndani ya dakika tano au hata pungufu, “ ungesema nini?
Ninyi ndio mmeitwa kufanya mambo kama haya kutokea. Ni wakati
wenu.
Je Boksi lako la vifaa lipo tayari?
Comments
Post a Comment